Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kutoka kulala mitaani hadi kumiliki duka la mikate Costa Rica

Kutoka kulala mitaani hadi kumiliki duka la mikate Costa Rica

Pakua

Nchini Costa Rica sera ya kuwezesha wakimbizi kufanya kazi imeleta nuru kwa raia wa Colombia waliokimbia machafuko nchini mwao. Flora Nducha na ripoti kamili.

(Taarifa ya Flora Nducha)

Miaka 17 iliyopita, ghasia nchini Colombia zilisababisha Miriam Velásquez na mumewe Ricardo Ángel kukimbia nchi yao na kusaka hifadhi nchini Costa Rica.

Baada ya kuwasili kwenye mji mkuu San Jose, familia hiyo haikuwa na kipato chochote na hivyo kujikuta wanaishi mitaani.

Hata hivyo hivi sasa maisha yao yamebadilika baada ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kuwapatia mtaji kidogo wa kufungua duka la kuoka mikate isiyo na protini.

Miriam anasema maisha yao yamebadilika.

(Sauti ya Miriam Velásquez)

 “Tulikuja na ari na bado tuna ari hiyo ya kuhangaika ili tufanye chochote, tufanye kazi na kusonga mbele.”

image
Ricardo Ángel mkimbizi kutoka Colombia ambaye sasa anatumia stadi zake za ujasiriamali kuoka mikate na kuuza huko Costa Rica. (Picha:UNifeed video capture)
Duka lao la kuoka mikate ni kubwa zaidi nchini Costa Rica ambapo mtaji waliopata walitumia kupata mafunzo na kununua vifaa na sasa wanasaka fedha zaidi ili mkopo wa aina hiyo uweze kunufaisha watu wengi zaidi.

(Sauti ya Miriam Velásquez)

 “Bila shaka hiki tulichofanya kinaweza kuwa mfano kwa wengine.”

Photo Credit
Familia hii kutoka Colimbia sasa inatumia stadi za ujasiriamali na imefungua duka kubwa zaidi la kuoka mikate isiyo na protini hatarishi huko Costa Rica. (Picha: © UNHCR/Santiago Escobar-Jaramillo)