Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP yapokea dola milioni moja kutoka China kusaidia wakimbizi Iran

WFP yapokea dola milioni moja kutoka China kusaidia wakimbizi Iran

Pakua

Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa, WFP limekaribisha  mchango wa dola milioni 1 kutoka China kwa ajili ya  chakula na pia vifaa vya  elimu kwa wasichana wakimbizi  wa Afghanistan na Iraq wanaoishi nchini Iran.

Negar Gerami ambaye ni mwakilishi wa WFP Iran amesema mchango huo ambao umefika muda muafaka  utasaidia kuongeza chakula kama vile mchele, unga wa ngano kwa ajili ya wakimbizi elfu 30 ambao hutegemea sana msaada kutoka WFP katika kujikimu mahitaji mbalimbali.

Kwa upande wake China imesema mchango huo ni sehemu ya utekelezaji wa mfuko wa usaidizi wa ushirikiano wa Kusini-Kusini uliotangazwa na Rais wa China Xi Jinping katika mkutano wa uendelezaji wa Umoja wa Mataifa wa Septemba 2015, ikiwa ni  jitihada za  usalama wa chakula kwa wakimbizi walioathirika sana nchini Afghanistan katika Iran.

Photo Credit
WFP yapokea dola mimioni moja kutoka serikali ya china kusaidia wakimbizi Iran. Picha: WFP