Neno la wiki: Harara
Pakua
Wiki hii tunaangazia neno “Harara” na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.
Bwana Sigalla anasema neno "Harara" lina maana nyingi, ya kwaza ni jinsi mtu anavyohisi kuwashwawashwa kwnye ngozi ya mwili, pili ni hali ya mtu kuwa na hasira mbaya ya ghafla, tatu ni hali ya mtu kutokwa na vipele kwenye ngozi, na ya nne ni mbambuko wa ngozi aghalabu kwa watoto au wanawake katika sehemu za mapaja kutokana na joto kali.