Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ubunifu wa nguo za magome ya miti na uhifadhi wa mazingira Burundi-sehemu 1

Ubunifu wa nguo za magome ya miti na uhifadhi wa mazingira Burundi-sehemu 1

Pakua

Katika  Juhudi za kuunda ajira na  kuhifadhi mazingira, msichana kutoka Burundi Annick Kabatesi ameanzisha mradi wa kutengeneza nguo zitokanazo na magome ya miti.  Nguo hizo zimetajwa kuwa zinazingatia uhifadhi wa mazingira. Bi. Kabatesi ambaye ni mwanamitindo pia amejijengea umaarufu mkubwa kwa  kutengeneza nguo hizo za magome ya miti  baada ya nguo hizo kuwavutia viongozi wakuu Serikalini.

Sambamba na mpango huo wa nguo za miti, mwanaharakati huyo wa mazingira  Annick Kabatesi ameanzisha  pia mpango wa kupanda miche  ya miti ili kurejeshea  miti inayokatwa kwa shughuli hiyo ya kutengeneza nguo kwa kutumia magome ya miti. Mwandishi  wetu  wa  Maziwa makuu  Ramadhani KIBUGA amezungumza na  Annick Kabatesi  kuhusu  mradi huo na katika sehemu hii ya kwanza anaangazia wanavyopata magome ya miti na kutengeneza kitambaa.

Photo Credit
Mwanaharakati wa mazingira Annick Kabatesi kutoka Burundi. Picha: Annick Kabatesi