Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hispania kushirikiana na UM katika kampeni ya usafi wa bahari

Hispania kushirikiana na UM katika kampeni ya usafi wa bahari

Pakua

Serikali ya Hispania imetangaza rasmi leo kuunga mkono Umoja wa Mataifa  katika kampeni ya usafi wa bahari katika hafla ya  mashindano ya bahari yajulinkanao kama Volvo ocean Race, yaliofanyika  Alicante.

Bw.Raquel Orts Nebot, ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya maendeleo ya pwani na Bahari nchini Hispania amethibitisha jitahada za taifa hilo kubwa na muhimu duniani kujiunga na nchi zingine 32 katika  kampeni ya umoja wa mataifa ya usafi wa bahari. Bw Raquel amesma serikali yake itakuwa mtari wa mbele katika kuzihimiza nchi zingine na asasi za kiraia katika kupunguza matumizi ya plastiki baharini.

Naye Erik Solheim mkurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingiria UNEP amesema  ushiriki wa Hispania katika kampeni hii unatuma ujumbe muhimu ukanda wa  mediterranean na duniani kote.  Ameongeza kuwa kama binadamu  tuna wajibu wa kulinda bahari maana ni muhimu kwa maisha yetu .

Ripoti ya  UNEP inasema uzalishaji wa plastiki umefikia zaidi ya  tani bilioni  8.3 duniani kote, na  mwaka 2015 tani bilioni 6.3 tayari zimetupwa, hivyo tani milioni 8 zinatupwa katika bahari zetu kila mwaka.

Watalaamu wanasema uchafuzi mwingi unajumuisha plastiki  kama vikombe, mifuko, majani, chupa  na  vipodozi... Na ifikapo mwaka  2050 imeelezwa kuwa  kutakuwa na plastiki zaidi katika bahari kuliko samaki.

Photo Credit
Taka zilizopo kando ya bahari. Picha: UM