Neno la Wiki: Mlipuko na Mkurupuko
Pakua
Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno "Mlipuko" na "Mkurupuko" Mchambuzi wetu ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.
Nuhu anasema neno "mlipuko" ni sauti ya ghafla ya kutisha ambayo inayotokana na moto au upasuaji ya mti na mengineyo, na neno "Mkurupuko" inatokana na neno kurupuka, ambalo linamaanisha kuamka kwa ghafla ama kutekeleza kitendo fulani kwa kushtukia au bila ya kupanga.