Neno la wiki- Mchuuzi na Machinga
Pakua
Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno Mchuuzi na machinga. Mchambuzi wetu ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA
Bwana Zuberi anasema kwamba mchuuzi ni mtu anyeuza vitu vidogo vidogo alivyoweka sehemu iwe ni matunda, vichana au mboga alimradi anuza kwa bei ya reja reja. Machinga ni mtu yule yule anayeuza vitu vidogo vidogo lakini badala ya kuviuza katika sehemu anavibeba na kuzungusha iwe ni barabarani au kwingineko.