Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Bila ushirikiano wetu hatutatimiza SDG's

Bila ushirikiano wetu hatutatimiza SDG's

Pakua

Kongamano la mwaka huu la Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa, ECOSOC kuhusu Ushirikiano limefanyika leo jijini New York, Marekani kujadili hatua za kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.

Akihutubia kwa njia ya video katika mkutano huo ulioleta pamoja wadau wa kimataifa, asasi za kiraia na makampuni binafsi, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bi. Amina Mohammed amesema, wakati wa kupitisha ajenda ya 2030, mataifa yalijua urefu wa kiwango chake, na vile vile yalifahamu kwamba hayawezi kuzifikia bila ushirikiano jumuishi na thabiti, akiongeza kuwa..

image
Bi. Amina Mohammed akalihutubia kongamano kwa njia ya video. Picha:UN Photo/Manuel Elias
(Sauti ya Amina)

"Kukuza ushirikiano fanisi kutahusisha mkazo zaidi katika ubunifu, athari, uwazi, mshikamano, uwajibikaji na uendelevu. Ni jambo muhimu sana katika juhudi zetu za sasa katika kuwezesha Umoja wa Mataifa kusaidia nchi kutimiza malengo ya 2030 na ahadi za mabadiliko ya tabianchi."

image
Rais wa Baraza Kuu Peter Thompson. Picha: UN Photo/Manuel Elias
Naye Rais wa Baraza Kuu Peter Thompson amesema kama bara la Afrika lenye asilimia 70 ya nchi za chini kimaendeleo, zenye misheni 9 kati ya 16 za ulinzi wa amani, na nusu ya watu ulimwenguni kote wanaishi katika umasikini uliokithiri, si budi kubadili utekelezaji ..

(Sauti ya Thompson)

"Ikiwa tunataka malengo ya maendeleo endelevu yapatikane katika kipindi cha miaka 13, na ikiwa tunataka matumaini yoyote ya mustakabali endelevu kwa ajili yetu wote, ni lazima tuachilie mbali malalamiko ya zamani na wasiwasi, na tuungane pamoja kwa nguvu katika fikra mpya, tushirikiane, tuwekeze kifedha, na kujitolea mashinani".

Photo Credit
UN Photo/Manuel Elías