Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNMISS yatembelea Kajo Keji kujionea hali halisi

UNMISS yatembelea Kajo Keji kujionea hali halisi

Pakua

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS unasema kuwa karibu wakimbizi wa ndani 1800 kwenye eneo la Kajo Keji nchini wanahitaji msaada wa dharura. Japokuwa wakimbizi hawa wamejipata kwenye kambi za wazi kwa muda mrefu lakini kuna nuru ya matumaini walipotembelewa na maafisa wa UNMISS na wale wa kutoka kwa shirika la kiserikali linalohusika na masuala ya maendeleo pembe ya Afrika, IGAD. Ungana na Flora Nducha akiangazia yanayoendelea kwenye eneo hilo....

Photo Credit
Kajo Keji Sudan Kusini. Picha: UM/Video capture