Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kutana na Erick David Nampesya, mwanahabari gwiji aliyekutana ana kwa ana na Guterres

Kutana na Erick David Nampesya, mwanahabari gwiji aliyekutana ana kwa ana na Guterres

Pakua

Akiwa na siku nne pekee ofisini tangu aanze majukumu yake , Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, ambaye aliapishwa mnamo Disemba 12 mwaka jana, anaelezwa na wengi kuwa mwenye mwelekeo sahihi wa kukivusha chombo anachokiongoza hususani katika utatuzi wa changamoto za kibinadamu.

Miongoni mwa watu wanaomfahamu ni Erick David Nampesya, mwanahabari mkongwe kutoka Tanzania ambaye alikutana na kumhoji kiongozi huyo miaka kumi iliyopita na anakumbuka vyema mazungumzo yao. Mwanahabari huyo anamweleza Joseph Msami wa idhaa hii kile kilichojiri.

Photo Credit
Erick David Nampesya.(Binafsi)