Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno la wiki- Behewa

Neno la wiki- Behewa

Pakua

Wiki hii tunaangazia neno Behewe na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania. Buhewa lina zaidi ya maana moja, maana ya kwanza ni mahali pa wazi katika nyumba, maana nyingine ni sehemu au ghala ya kuwekea bidhaa kisawa chake ni bohari na nyingine ni sehemu ya gari moshi ya kuchukuliwa abiria au bidhaa.

Photo Credit
Picha:Idhaa ya Kiswahili