Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban alaani shamulio dhidi ya shule Aleppo

Ban alaani shamulio dhidi ya shule Aleppo

Pakua

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amelaani vikali mashambulizi dhidi ya shule mashariki mwa mji wa Aleppo nchini Syria hii leo ambayo yamesababaisha vifo vya watu kadhaa.

Taarifa ya msemaji wa Katibu Mkuu, imemnukuu Ban akisema matuko kama mashambulizi hayo yamefanywa kwa kukusudia yaweza kuchochea uhalifu wa kivita.

Amesema wahusika wa vitendo hivyo lazima wafikishwe katika mkono wa sheria na kusisistiza wito wake kwa Baraza la Usalama kupelekea suala la Syria katika mahakama ya kimtaifa ya uhalifu, ICC.

Photo Credit
Watoto wakirudi kutoka shuleni mjini Aleppo Syria. Picha ya UNICEF/UN06848/Al Halabi