Neno la wiki-papa
Pakua
Katika Neno la Wiki hii Ijumaa Juni 10 tunaangazia neno papa na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, huko nchini Tanzania.
Onni Sigalla anazungumzia matumizi ya neno papa. Anasema papa ni kiongozi mkuu wa kanisa ya katoliki. Pia papa inamaana ya samaki mkubwa ambaye ana mdomo mkubwa na huzaa badala ya kutaga mayai.Aidha papa ina maana ya moyo kwenda mbio kutokana na hofu au kupungua kwa maji kwa mfano katika chungu lisilokuwa na tundu. Maana nyingine ya papa ni kuonyesha sip engine mbali ni pale alipo mzungumzaji yaani papa hapa.