Ugonjwa wa Kisukari Tanzania na harakati za kuutokomeza
Pakua
Ugonjwa wa kisukari unamulikwa katika maadhimisho ya kimataifa ya siku ya afya yanayoadhimishwa leo tarehe saba mwezi Aprili.
Takwimu za shirika la afya ulimwenguni WHO zinaonyesha kuwa Idadi ya watu wanaoishi na kisukari imeongezeka takribani mara nne tangu mwaka 1980 na kufikia watu wazima milioni 422.
Barani Afrika hali ikoje? Tuelekee Tanzania ambapo Anatory Tumaini a redio washirika Karagwe Fm ya Kagera nchini humo ametuandalia makala ifuatayo