Kama si redio majanga hutuacha segemnege: Wananchi Tanzania
Pakua
Katika mfululizo wa makala kuhusu umuhimu wa redio katika majanga ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya redio duniani Februari 13, leo tunajikita nchini Tanzania ambako wakazi wa Mwanza wanaeleza namna redio ilivyokuwa kiungo muhimu katika kuwapasha taarifa wakati wa majanga.
Ungana na msimulizi Hemed Mohamed katika makala iliyotayarishwa na Dotto Bulendu wa redio washirika Redio SAUT ya Mwanza Tanzania.