Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utapiamlo ni miongoni mwa masaibu ya watoto wakimbizi kutoka Burundi

Utapiamlo ni miongoni mwa masaibu ya watoto wakimbizi kutoka Burundi

Pakua

Mwezi mmoja baada ya mmiminiko wa kwanza wa zaidi ya wakimbizi 55,000 huko mkoani Kigoma,  Kaskazini Magharibi mwa Tanzania, kufuatia hali ya shuka panda  ya kiusalama nchini Burundi. watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano wako hatarini kuugua utapiamlo na wanahitaji msaada wa kibinadamu wa dharura. Habari hizo zinawekwa bayana wakati ambapo zaidi ya asilimia 60 ya wakimbizi katika kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma ni watoto.Je hali ikoje? Ungana na Joseph Msami katika makala hii.

Photo Credit
Mama na mwanae waliokimbilia nchini Tanzania.(Picha ya UM/Unifeed)