Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakimbizi zaidi wa Burundi wawasili Uvira

Wakimbizi zaidi wa Burundi wawasili Uvira

Pakua

Tangu kuanza kwa mzozo wa kisiasa nchini Burundi, tarehe 25 Aprili, siku ambapo rais Pierre Nkurunziza ametangazwa kuwa mgombea rais wa chama tawala, zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makwao na kutafuta hifadhi kwenye nchi jirani, ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, ni zaidi ya wakimbizi 9,000 waliofika kwenye eneo la Uvira, Kivu Kusini.

Wakati UNHCR inaandaa eneo maalum kwa kuwapiatia hifadhi, jamii iliyopo Uvira imekubali kuwapokea wakimbizi hawa.

Ungana na Priscilla Lecomte kwenye makala hii.

Photo Credit
Wakimbizi wa Burundi wakifika Uvira. Picha ya UNHCR.