Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Capoeira ya Brazil yaleta ahueni kwa watoto waliotumikishwa DRC

Capoeira ya Brazil yaleta ahueni kwa watoto waliotumikishwa DRC

Pakua

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mzozo Mashariki mwa nchi hiyo umetumbukiza watoto na vijana katika kutumikishwa vitani. Hata hivyo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linahaha kila uchao kuwanasua watoto hao kutoka mikono ya watumikishaji.

Baada ya kuwanasua, UNICEF huwaweka vijana katika kambi ya mpito ili kuwapatia stadi za maisha na waweze kutengamana na jamii na miongoni mwao ni ile iliyoko Goma ambako vijana huishi kwa muda wa wiki tano. Je hufanya nini? Kwa undani ungana na Assumpta Massoi kwenye Makala hii.

Photo Credit
Mchezo wa capoeira, picha ya UNICEF.