Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hata baada ya 2015 tuna wajibu wa kutimiza malengo yaliyosalia:Mwinyi

Hata baada ya 2015 tuna wajibu wa kutimiza malengo yaliyosalia:Mwinyi

Pakua

Waziri wa afya wa Tanzania Dr Hussein Mwinyi amesema pamoja na serikali ya Tanzania kutimiza lengo la nne la milenia ambalo ni kupunguza vifo vya watoto wa chini ya miaka mitano, taifa hilo bado lina wajibu wa kuhakikisha malengo mengine yaliyosalia yanatimizwa hata baada ya ukomo wa malengo hayo mwaka 2015.

Akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Radio ya Umoja wa Mataifa Mwinyi amesema wamewasilisha mapendekezo yao kwenye baraza kuu ya kutana kutimiza malengo yaliyosalia na pia kuunda malengo mapya. Ameketi na Flora Nducha kufafanua yote hayo akianza na malengo yahusuyo afya

(MAHOJIANO NA DR MWINYI)