METHALI: Achekaye kovu hajaona jeraha
Leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunakupeleka Baraza la Kiswahili la Taifa, Zanzibar, BAKIZA kwake Katibu Mtendaji Dkt. Mwanahija Ali Juma akifafanua methali “ACHEKAYE KOVU HAJAONA JERAHA.”
Leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunakupeleka Baraza la Kiswahili la Taifa, Zanzibar, BAKIZA kwake Katibu Mtendaji Dkt. Mwanahija Ali Juma akifafanua methali “ACHEKAYE KOVU HAJAONA JERAHA.”
Katika kujifunza Kiswahili, leo mtaalam wetu Onni Sigalla Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, anatufafanulia maana ya msemo "FUNGA FUNGANYA", karibu!
Katika kujifunza Kiswahili mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania , anatufafanulia maana ya msemo "FANYA ILHAM". Karibu!
Katika kujifunza kiswahili tutasikia maana ya methali “USISHINDANE NA KARI, KARI NI MJA WA MUNGU”na mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani. Anaanza kwa kusema kari ni neno linalotokana na neno "karima" au "karama", ambalo linamaanisha zawadi au kipawa maalum kutoka kwa mwenyezi Mungu, ama kweli usishindane na mwenzako, tosheka na kari yako maana yote yatoka kwake mwenyezi Mungu!
Hii leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili, mchambuzi wetu Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi katika Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anaeleza maana ya misemo na anachambua misemo miwili; 'andaa meza' na 'ndoa imejibu." Karibu
Na leo katika kujifunza Kiswahili, mchambuzi wetu ni Dkt Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA, anatufafanulia maana ya methali "Usigombane na mkwezi, nazi imeliwa na mwezi", karibu!
Na sasa ni wakati wa kujifunza Kiswahili, ambapo leo mtaalam wetu Onni Sigalla Mhariri Mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, anatufafanulia maana ya neno "MUKU"
Na leo katika kujifunza Kiswahili, mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anatufafanulia maana ya methali, "MWANZO KOKOCHI MWISHO NAZI," karibu!
Leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili mtaalam wetu hii leo ni Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA anachambua methali, Mchama ago Hanyele, huenda akawia papo.
Hii leo katika kujifunza lugha ya kiswahili tunakwenda Zanzibar nchini Tanzania ambako Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA Dkt. Mwanahija Ali Juma anachambua methali isemayo "Paka hakubali kulala chali." Karibu!