Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Neno La Wiki

UN News Kiswahili

Neno la wiki - Bumbuwazi

Katika neno la wiki hii leo tunaangazia neno "Bumbuwazi". Mchambuzi wetu  ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA . 

Bwana Nuhu anasema unapopigwa na butwaa ama kupatwa na mshangao, hadi ukawa huwezi kuongea hata neno moja basi utakuwa umepigwa na bumbuwazi.

Sauti
13"
UN News Kiswahili

Wafahamu maana ya neno Mlaso? Ungana na Onni Sigalla

Wiki hii tunaangazia neno “Mlaso” na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema Mlaso ni aina ya chakula kinachoandaliwa mama ambaye amejifungua ili aweze kuwa na maziwa ya kutosha na kurudisha afya yake.  Maeneo mengine huchanganya chakula hicho aghalabu na damu au maziwa.

Sauti
32"

Neno la wiki - Ndongosa

Wiki hii tunaangazia neno "Ndongosa" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema neno “Ndongosa” ni ng'ombe wa kike ambaye anatoka kwenye hali ya undama kuingia ukubwa lakini bado hajapandwa.

Neno la Wiki- Mhanga, Manusura na Muathirika

Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno “Mhanga”, "Manusura" na “Muathirika”.  Mchambuzi wetu  ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.

Ungana naye upate matumizi sahihi ya maneno hayo..

Sauti
58"

Neno la wiki: Mhanga, Manusura na Muathirika

Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno "Mhanga", “Manusura” na "Muathirika".  Mchambuzi wetu  ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.

Ungana naye upate matumizi sahihi ya maneno hayo..

Neno la Wiki: tofauti za Supu na Mwengo ni zipi?

Wiki hii tunaangazia maneneno "Supu” na “Mwengo" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema sio kila kitu ambacho kimepikwa katika maji ni Supu. Mwengo ni aina ya supu itokanayo na kupika viumbe vya bahari kwa maji, kama vile samaki, pweza, ngisi. Ukitaka kuagiza supu yake unasema naomba mwengo wa samaki, mwengo wa pweza au mwengo ya ngisi…

Sauti
48"

Tofouti za Supu na Mwengo ni zipi?

Wiki hii tunaangazia maneneno “Supu" na "Mwengo” na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema sio kila kitu ambacho kimepikwa katika maji ni Supu. Mwengo ni aina ya supu itokanayo na kupika viumbe vya bahari kwa maji, kama vile samaki, pweza, ngisi. Ukitaka kuagiza supu yake unasema naomba mwengo wa samaki, mwengo wa pweza au mwengo ya ngisi...

Neno la Wiki: Halisi, Uhalisi, Uhalisia

Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno "Halisi", “Uhalisi” na "Uhalisia".  Mchambuzi wetu  ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.

Ungana naye upate matumizi sahihi ya maneno hayo, ambayo hutumiwa ndivyo sivyo…

Sauti
1'11"

Neno la Wiki: Halisi, Uhalisi, Uhalisia

Katika neno la wiki hii leo tunaangazia maneno “Halisi”, "Uhalisi" na “Uhalisia”.  Mchambuzi wetu  ni Nuhu Zuberi Bakari, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa masuala ya mawasiliano kwenye Chama cha  Kiswahili cha Taifa nchini Kenya, CHAKITA.

Ungana naye upate matumizi sahihi ya maneno hayo, ambayo hutumiwa ndivyo sivyo...

Je wafahamu maana ya neno mzimu?

Wiki hii tunaangazia neno "Mzimu" na mchambuzi wetu ni Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi, katika Baraza la Kiswahili la Taifa, BAKITA, nchini Tanzania.

Bwana Sigalla anasema neno “Mzimu” lina maana zaidi ya moja. Maana ya kwanza ni mahali pa kufanyika matambiko ambayo ni chini ya miti mikubwa kama mbuyu au mkuyu au hata kwenye mapango. Maana ya pili ni kivuli cha sura ya mtu ambaye amefariki dunia. Maana ya tatu ni maskani ya watu waliofariki dunia kama vile makaburini ambako watu wanaweza kwenda kufanya mawasiliano na ndugu zao waliofariki dunia.