Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UNCDF

Hatua zachukuliwa kudhibiti athari za COVID-19 kwa wanawake, Uganda

Mlipuko wa COVID-19 tangu ulipoanza umesambaratisha matumaini ya wengi kiuchumi na kijamii kutokana na vikwazo vya usafiri na biashara nyingi zikipigwa marufuku kama njia ya kudhibiti mlipuko huo. Wanawake na wasichana wameathirika zaidi kutokana na hali yao ya uhaba wa rasilimali hali ambayo pia imechochochea vurugu za nyumbani na ukatili wa kijinsia kwa mujibu wa ripoti za serikali mbalimbali.

Sauti
3'44"
© UNICEF/Schermbrucker

Muhimu ni kuwaambia watu sababu ya kwa nini unawaambia wapande miti-Dr Kalua

Nchi nyingi duniani hususan za afrika zinakumbwa na changamoto kubwa za kutunza mazingira. Mara nyingi hili hutokana na watu kutohamasishwa vya kutosha kuhusu manufaa yatokanayo ya utunzaji wa mazingira. Wakfu wa Green Africa ulioanzishwa mwaka 2000 umekuwa kwenye mstari wa mbele kuhakikisha kuwa watu wamepata kuelewa umuhimu wa utunzaji mazingira Barani Afrika na hata wameanzisha mradi ufahamikao kama 'Plant your age' yaani panda miti idadi sawa na umri wako. Mwandishi wa Kenya Jason Nyakundi amezungumza na muasisi wa wakfu huo wa Green Africa Dr Isaac Kalua.
Sauti
5'33"
Picha: UNICEF/Al-Zikri

Vijana waonywa dhidi ya matapele wanaposaka ajira katia sekta ya mafuta, Uganda

Kutokana na kiwango kikubwa cha ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana katika nchi nyingi duniani, baadhi ya vijana wamejikuta katika mazingira ya kunyang’anywa kidogo walichonacho kupitia mikono ya matapeli.

Hali si tofauti nchini Uganda mabapo uzalishaji wa mafuta unanyemelea katika Bonde la Ufa la Ziwa Albert.

Taarifa zinasema tayari vijana kadhaa wamekuwa waathirika wa utapeli kwa kulipa pesa kama moja ya masharti ya kupata kazi mbalimbali katika makampuni ya mafuta yaliyoanza upya kufanya kazi baada ya kusitishwa kutokana na mlipuko wa COVID-19.

Sauti
3'53"
UN Tanzania/Ahimidiwe Olotu

Kumhoji Rais alikuwa anatumwa mwandishi mwanaume badala ya mwanamke-Bi.Mongela

Bi Getrude Mongela kupitia katika mahojiano yaliyofanywa na Stella Vuzo wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Tanzania, mwanamke huyo aliyekuwa Katibu Mkuu wa mkutano wa 4 wa wanawake uliofanyika Beijing miaka 25 iliyopita, anaeleza mafanikio ambayo yamefikiwa katika kumpa nafasi mwanamke, akianza na mfano hali ilivyokuwa awali katika vyombo vya habari.

Sauti
3'31"
UN/Andrew Kahwa

Mazingira yamefanya familia yangu ipate lishe bora na kipato-Mfugaji wa Sungura Tanzania

Bi Joyce Ballo wa Ifakara Morogoro Tanzania, anasema uamuzi wa wakulima wa mbogamboga na miti katika eneo lake wa kutumia njia mbadala za kutunza mazingira kwa kuamua kutotumia dawa na mbolea zenye sumu, kumempa fursa ya kupata kipato na lishe kwa familia yake. 

 

Kupitia katika mahojiano haya yaiyofanywa na John Kabambala wa redio washirika KidsTime FM ya Morogoro, mkulima huyo anaeleza uhusiano wa utunzaji mazingira na chanzo chake cha sasa cha kipato, yaani ufugaji wa sungura ambapo anaweza kuingiza takribani dola 15 kwa wiki kutokana na shughuli hiyo. 

Sauti
3'36"
UN Photo/Rick Bajornas)

Watu wanafikiri Umoja wa Mataifa ni shirika moja tu-Balozi Manongi

Jumapili hii ulimwengu unaadhimisha siku ya Umoja wa Mataifa ambayo mwaka huu inabeba kilele cha maadhimisho ya Umoja huo kutimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1945. Umoja huo umepitia katika mabonde na milima mingi lakini lengo lake kuu la kutunza amani ya ulimwengu na kupafanya mahali bora pa kuishi limeendelea pasina kutetereka. 
 
Balozi Tuvako Manongi, mwanadiplomasia aliyebobea na aliyepata kuwa Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa anaeleza faida za Umoja wa Mataifa kwa ulimwengu hususani kwa nchi zinazoendelea. 
Sauti
3'36"
World Bank / Sarah Farhat

Mabaraza ya watoto Tanzania yalianzishwa ili kuwashirikisha watoto katika kupanga mstakabali wao

Ni wazi kwamba ili kujenga jamii iliyo bora, ni muhimu kuanzia chini katika mizizi ya jamii yaani kuwaelimisha watoto kuhusu wajibu na haki zao. Lakini ni wazi pia kuwa lengo hilo linaweza kufanikiwa kwa ufanisi zaidi ikiwa watoto wenyewe watashirikishwa kuanzia ngazi ya awali kwa wao wenyewe kutoa maoni yao na pia kupata fursa nyingine kama za kuwa na mahali pa kutoa taarifa iwapo haki zao za utoto na kijamii zinapokwa na hivyo kuathiri ustawi wao.

Sauti
4'2"
UN News/Assumpta Massoi

Licha ya changamoto, mwanamke wa kijiji bado anajitahidi kujikwamua

Hivi karibuni dunia imeadhimisha siku ya mwanamke wa kijijini ikimulika harakati zao na changamoto wanazokumbana nazo hasa wakati huu wa janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19. Kundi hili limegubikwa na changamoto kama vile huduma za kijamii na kiuchumi na hivyo janga la COVID-19 kuwa sawa na kuongeza chumvi kwenye kidonda.

Audio Duration
3'54"
UN News/ John Kibego

Ugunduzi wa rasilimali ya mafuta huwa ni wa kujivunia lakini unakuja na changamoto zake

Ugunduzi wa rasilimali ya mafuta hua ni wa kujivunia kwani huleta fursa nyingi zikwemo ajira, ukwaji wa miji, viwanda na hata uchumi wa taifa kwa ujumla.

Lakini kwa upande mwingine hua na madhara kwa mazingira na jamii ambayo huathiri zaidi watu wa kipato cha chini katika jamii husika.

Uganda inajiandaa kuanza kuzalisha mafuta katika eneo la Bonde la Ufa la Ziwa Albert ambapo sasa wanamazingira wanaonya kuhusu athari za viwanda vya mafuta wakati ambapo misitu ya asili inazidi kuchafuliwa kwa ajili ya kilimo na makaazi.

Je, wanasema ini?

Sauti
3'50"