Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UNMISS/Eric Kanalstein

Kupitia asali nimeweza kuwapatia wanawake na vijana shughuli ya kipato

Msichana Joreen Wanini wa nchini Kenya, mfanyabiashara ya asali ambaye amefikia hatua ya kuwa chanzo cha ajira kwa watu wengine hususani wanawake na vijana, anawaambia vijana wenzake wawekeze kwenye kilimo na mazao ya kilimo kwani mara zote watu watahitaji chakula na itakuwa chanzo cha ukuaji wa uchumi katika jamii.

Joreen alijiajiri mara tu baada ya kumaliza masomo yake akinunua asali kutoka kwa wakulima wadogowadogo na kuiongezea thamani kwa kuiweka katika vifungashio vizuri kisha kuuza kwa watu wengine wenye uhitaji hasa katika kipindi cha mlipuko wa ugonjwa wa Covid-19.

Sauti
3'46"
© World Bank/Arne Hoel

Mradi wa ufugaji wa sungura na kuku wae ndelea kutumika kupamba na udumavu Tanzania

Lishe duni kote duniani ni tishio kubwa kwa ustawi wa binadamu kutokana na uhaba wa chakula kwa upande mmoja, na wakati mwingine ukosefu tu wa elimu kuhusu matumizi bora ya vyakula vinavyopatikana katrika jamii. Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu, SDGs, kwa namna tofauti tofauti yanalenga pamoja na mambo mengine, kuliondoa tatizo hili ili kuwaokoa afya za watu hususani watoto duniani kote.

Sauti
3'27"
John Kibego

Uganda yaimarisha utoaji chanjo dhidi ya COVID-19

Serikali ya Uganda imeamua kushirikiana zaidi na wadau mbalimbali ikiwemo makampuni ya mawasilaino na yale ya vinywaji katika juhudi za kuimarisha chanjo dhidi ya COVID-19.

Kampuni ya bia ya Nile Breweries imelivalia njuga suala la kuhamasisha wateja wake kupata chanjo hiyo itakayotegemewa na serikali ili kufungua sekta yao iliyofungwa tangu mwaka jana na zingine. Je, kampeni hiyo inatekelezwaje? Na mtazamo wa raia wa Uganda kuhusu chanjo huyo ukoje sasa?

Mwandishi wetu wa Uganda John Kibego anaripoti.

 

Sauti
3'52"
UN/ John Kibego

Jamii ya Watyaba kandoni mwa Ziwa Albert nchini Uganda yatishiwa tena na mafuriko

Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP26 unaendelea katika huko Glosgow na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiwa amewaeleza viongozi wa ulimwengu kuwa ni muhimu kuchukua hatua sasa kwani wanadamu wanajichimbia kaburi, nchini Uganda jamii ya Watyaba, mojawapo ya jamii za walio wachache wanaoishi katika viunga vya Ziwa Albert, wanapaza sauti kwa serikali na shirIka  la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kuwasaidia kutokana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
3'45"
TAHA

UNDP na TAHA nchini Tanzania wajenga vituo vitano vya kuhifadhi na kufungasha mazao

Umoja wa Mataifa unapigia chepuo mifumo sahihi ya chakula inayolenga kuongeza mnyororo wa thamani kuanzia shambani hadi kwa mlaji. Hatua hii siyo tu inasaidia kutokomeza njaa bali pia inaongeza kipato kwa mkulima na ustawi kwa mlaji kwa kuwa zao ambalo linapatikana eneo moja la dunia linaweza kusafirishwa katika ubora wake na kufikia eneo lingine la dunia katika ubora huo huo.

Sauti
7'56"
© UN-Habitat /Julius Mwelu

Tunaandaa mashindano mbalimbali ya michezo ili kuwaondoa vijana kwenye mawazo mabaya - ETCO

Mara kwa mara Umoja wa Mataifa umeendelea kusisitiza kuwa vipaji vikiwemo vya michezo vina mchango mkubwa katika kusaidia kuleta maendeleo na amani.

Vijana wanapotambuliwa vipawa vyao wanapata shughuli rasmi za kufanya na hivyo kuinua vipato vyao, kuwaondoa katika mazingira hatarishi na faida nyingine za ujumla ambazo muunganiko wake unasaidia kuelekea katika kutimiza malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.

Sauti
3'7"
© UNFPA Myanmar/Yenny Gamming

Wazazi tulinde watoto wetu dhidi ya mimba katika umri mdogo - Catherine Kobusinge Kamanyire

Nchini Uganda ripoti kutoka wilaya mbalimbali zinaonesha ongezeko la idadi ya wasichana waopata mimba utotoni kuliko wakati wowote kabla ya shule kufungwa kutokana na COVID-19. Wakati wilaya ya Hoima pekee imeripoti mimba za utotoni zaidi ya 6,000 wilaya jirani ya Masindi imeripoti zaidi ya wasichana 1,500 waliopata mimba kati ya mwezi Januari na Juni mwaka huu.

Uganda ina takribani wilaya 135.

Sauti
3'53"
Stephan Gladieu/World Bank

Mradi wa Benki ya Dunia waleta tumaini kufikia ajenda 30, Uganda

Mradi wa kuhakikisha maendeleo endelevu katika eneo lenye rasilimali ya mafuta nchini Uganda umeleta matumaini ya kukabili umaskini baada ya masoko kujengwa na barabara kadhaa katika wilaya tatu za eneo hilo.Je, mradi huo wa ARSDP unaofadhiliwa na Benki ya Dunia unasaidiaje? Basi ungana na mwandishi wetu wa Uganda John Kibego ambaye emezungumuza na viongozi wa mitaani kwenye ziara ya ukaguzi ya waziri wa maendeleo ya miji. 

Sauti
3'26"