Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

UN News/Anold Kayanda

Siku ya Kiswahili Duniani ni zawadi ya Tanzania kwenda duniani: Balozi Gastorn

Kutangazwa kuwa na siku maalum ya kuadhimisha lugha ya Kiswahili duniani ni zawadi kubwa kutoka Tanzania kwenda duniani na hii ni furaha kubwa sana amesema mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Profesa Kennedy Gastorn akielezea hisia zake baada ya wiki iliyopita shirika la elimu sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO kupitisha azimio la kuifanya tarehe 7 Julai kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani. 
(CLIP BALOZI KENENDY) 

UN Photo/Violaine Martin (file)

Mahojiano na Katibu Mkuu wa UN

“Ni wakati wa kupiga kengele ya dharura”, amesema Katibu Mkuu wa UN katika mahojiano maalum na Idhaa ya Umoja wa Mataifa siku chache kabla ya kuanza kwa Mjadala wa Juu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Akihojiwa na Assumpta Massoi wa UN News, António Guterres amegusia ushirikiano wa kimataifa, harakati za utoaji wa chanjo dhidi ya COVID-19 duniani, mabadiliko ya tabianchi, usawa wa jinsia, viijana, amani na usalama barani Afrika na duniani kwa ujumla

Sauti
9'34"
UN News

Mahojiano la Mbunge Neema Lugangira kutoka Tanzania kuhusu nafasi ya mbunge kwa umma

Uwepo wa wabunge wenye nguvu ni msingi imara wa Demokrasia kwani wawakilisha hao wa wananchi wanakuwa na uwezo wa kupitisha sheria, kutenga fedha kwenda kufanya kazi ya utekelezaji wa sheria na sera walizozipitisha na kuwajibisha serikali iwapo haijatenda yale wananchi wanayakusudia kwakuzingatia makundi yote kwenye jamii hususan walioko kwenye mazingira magumu. 

Wabunge pia wanajukumu la kuunganisha masuala ya nchi zao na masuala ya kimataifa na hivyo hupitia na kupitisha mikataba na maadhimio ili kufanya dunia iwe mahali salama na yenye kuwanufaisha wanadamu wote.

Sauti
8'51"
UN Tanzania

Mwanamke, kwenye uongozi huletewi kadi kama harusi - Balozi Getrude Mongela.

Mwanamke, kwenye uongozi huletewi kadi kama harusi - Balozi Getrude Mongela.

Kikao hiki cha 65 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani  CSW65 kilichoanza tarehe 15 Machi kikiwa sasa kinakamilisha wiki yake ya kwanza, wadau kwa namna mbalimbali kote duniani wanaendelea kujadili mada ya mwaka huu ambayo imejikita kwenye kuangazia wanawake katika uongozi ili kufikia dunia yenye usawa. 

Sauti
6'44"
UN Tanzania

Tenda wema nenda zako, msichana Aneth ambaye kitendo chake kimeendelea kuwasaidia wanafunzi viziwi, Chuo Kikuu cha Dare es Salaam

Katika mahojiano kati ya Ahimidiwe Olotu wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa na Aneth Gerana Isaya, msichana kiziwi ambaye ushauri wake alioutoa alipojiunga katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, umeendelea kuwasaidia viziwi wote wanaojiunga kwa masomo katika Chuo hicho kikongwev cha elimu ya juu nchini Tanzania. Aneth pia ni Mwanzilishi wa shirika la Furaha kwa Wanawake Viziwi Tanzania FUWAVITA. Aneth Isaya anaanza kwa kueleza hatua ambazo wameshapiga katika harakati za kupigania usawa wa kijinsia hususani kwa wanawake wenye ulemavu.

Sauti
6'51"
UN News

Ulemavu sio kulemaa tunachotaka ni kujumuishwa: Mbunge Mollel

Siku hii ya kimataifa ya watu wenye ulemavu inapoadhimishwa kote duniani watu wenye ulemavu wamekuwa wakipaza sauti zao kila kona kwamba ulemavu sio kulemaa wanachohitaji ni ujumuishwashi na miundombinu Rafiki itakayowawezesha kushiriki katika kusongesha mbele ajenda ya maendeleo endelevu kama wengine.

Miongoni mwa watu hao ni mbunge Amina Mollel kutoka nchini Tanzania,  yeye mwenyewe ni mlemavu na anawakilisha watu wenye ulemavu wa taifa hilo bungeni, akizungumza nami kwa njia ya simu kutoka mjini Arusha amesisitiza nafasi ya wenye ulemavu katika ujumbe wake.

 

Sauti
5'35"