29 JANUARI 2024
Hii leo kwenye Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa Anold Kayanda anaanzia na masuala ya afya, hususan viambato vya mafuta vinavyohatarisha afya ya mwili, kisha miradi ya UN ilivyosaidia wanawake huko Syria .Makala inakupeleka Angola kuona jinsi Umoja wa Mataifa umenusuru wanawake wa vijijini kwa hohehahe na mashinani atakupeleka katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma iliyoko Kaunti ya Turkana, nchini Kenya kupata ujumbe kuhusu elimu hasa kwa wasichana.
26 JANUARI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia maamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ vitendo vya mauaji ya kimbari katika mashambulizi ya Israel dhidi ya wapalestina huko Gaza. Pia tunamulika viwanda vya nishati safi ulimwenguni, makala ikitupeleka nchini India. Mashinani tnakuletea ujumbe wa mhamiaji ambaye ni mchezaji wa musiki, mwalimu na rafiki nchini Burundi.
Hata mimi mwenyewe nilikuwa sijiamini hadi nilipopata mafunzo ya RLabs - Mariam
Mkakati wa Afya ya Uzazi kwa Wasichana, Haki, na Uwezeshaji nchini Tanzania (GRREAT) unaoungwa mkono na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) kwa kushirikiana na wadau likiwemo shirika lisilo la kiserikali la RLabs Tanzania na serikali ya Canada ni mpango wa miaka mitano (2019-2024) ili kuisaidia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuboresha ustawi wa wasichana balehe katika mikoa ya Mbeya na Songwe, pamoja na Zanzibar.
19 JANUARI 2024
Hii leo jaridani tunaangazia vita katika ukanda wa Gaza, na tukielekea siku ya elimu duniani tunabisha hodi nchini Burundi ambako UNICEF inahakikisha watoto wakimbizi wanaorejea nchini humo wanaweza kuendelea na elimu. Makala na mashinani tunasalia na mada ya elimu bora na tunakupeleka nchini Uganda, kulikoni?.