Mwanadiplomasia wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa ili kuleta mustakabal mwema hasa katika kipindi hiki cha mpito nchini Libya, ambacho kinashuhudia kuzuka kwa vita vya kikabila vyama vya kirai vinawajibika kutoa mchango mkubwa kufanikisha ujenzi wa enzi za siasa mpya nchini humo.