Kisa kipya cha Ebola chathibitishwa Liberia:WHO
Shirika la afya ulimwenguni WHO limethibitisha kisa kipya cha homa kali ya Ebola nchini Liberia, kufuatia kifo cha mwanamke mwenye umri wa miaka 30 aliyefariki dunia jana mchana wakati akihamishiwa hosipitali mjini Monrovia.