Vichwa vya Habari
Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Amani na Usalama
Tangazo la Marekani na Iran la sitisho la mapigano kwa wiki mbili, yatarajiwa kuwa litawezesha kufunguliwa kwa mlango wa bahari wa Hormuz, njia muhimu ambamo kwayo moja ya tano ya nishati ya mafuta na gesi duniani hupitia kwa kutumia meli.
Habari kwa Picha
Wimbi kubwa zaidi la mashambulio ya Israel dhidi ya Lebanon
Mji mkuu wa Lebanon, Beirut, pamoja na viunga vyake, umekumbwa na mashambulio ambayo shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR, limeelezea kama "wimbi kubwa zaidi la mashambulizi ya Israeli hadi vita vianze."
Habari Nyinginezo
Afya
Madaktari na wahudumu wa afya katika ukanda wa Gaza eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu na Israel wanaonya kuwa mfumo wa afya katika eneo hilo sasa uko karibu zaidi kuporomoka kuliko wakati mwingine wowote, huku idadi ya wagonjwa ikiendelea kuongezeka, magonjwa ya ngozi na ya kupumua yakienea, na uwezo wa kuwahudumia watu wenye magonjwa sugu ukiendelea kupungua.
Utamaduni na Elimu
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF kwa kushirikiana na Benki ya Dunia linaendelea kurejesha matumaini ya elimu kwa maelfu ya watoto katika Jimbo la Mto Nile nchini Sudan kupitia Programu za Elimu Mbadala (ALP), baada ya miaka mingi ya vurugu na kusitishwa kwa masomo kuathiri mustakabali wao. Feissal Kirwa anaangazia zaidi.