Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Tabianchi na mazingira
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira UNEP limesema kuwa licha ya ongezeko la joto duniani kuendelea kutishia sayari, maendeleo ya teknolojia safi yanatoa matumaini mapya katika juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Habari kwa Picha
Miaka minne ya utumishi wa Joyce Msuya ndani ya UNOCHA
Joyce Msuya, Naibu Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu misaada ya dharura, OCHA anatamatisha jukumu lake baada ya kuhudumu kwa miaka minne. Ndani ya muda huo wa uongozi wake ametembelea zaidi ya nchi 30 na amekuwa akizungumza na watu katika shida na matumaini, umefanya takribani mikutano 20 na wanafunzi katika nchi mbalimbali na alipokuwa akirejea Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani aliongea na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa zaidi ya mara 40 ukiwa ni wastani wa karibia mara moja kila mwezi kueleza yale aliyoshuhudia mashinani pamoja na namna ofisi yake inavyowasadia wananchi. Hizi ni chache kati ya maelfu ya picha zinazoonesha akitekeleza majukumu yake.
Habari Nyinginezo
Afya
Upimaji wa mapema na ufuatiliaji vinasaidia
DRC waliothibitika na ugonjwa wamefikia 550
Vifo 101 DRC
Tabianchi na mazingira
Kesho kutwa Alhamisi ya Juni 11, macho na masikio yanaelekezwa Mexico, Canada na hapa Marekani kwa ajili ya fainali za kombe la dunia kwa mpira wa miguu, au soka al maarufu kabumbu. Ingawa hivyo zama za sasa za mchezo huo maarufu zaidi duniani zinakumbwa na madhara ya athari za mabadiliko ya tabianchi. Ongezeko la joto kali linavuruga mechi na kuzua wasiwasi kuhusu mustakabali wa mchezo huo. Ni kwa kuzingatia hilo, Sekretarieti ya Mkataba wa Kimataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi, UNFCCC inamulika suala hilo na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike kwani hivi sasa madhara ya joto kali kwenye kabumbu ni dhahiri.