Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Tabianchi na mazingira
Wiki ya pili baada ya Kimbunga Melissa kupiga magharibi mwa Jamaica, mitaa ya Savanna-la-Mar na Watercress bado ipo kimya, kimya cha mji unaojaribu kujikwamua na Athari zilizoachwa na zahma hiyo. Nyumba zimebomoka, shule zimeharibiwa, maisha yamepinduliwa. Makadirio yanaonesha kuwa watu milioni 1.6 wameathirika, na sasa timu za misaada zinafanya kazi kwa haraka usiku na mchana kutoa msaada muhimu wa chakula, makazi, na usalama.
Habari kwa Picha
Mradi wa UNEP umesaidia wakulima Gambia kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ili kuzuia wimbi la vijana wanaoondoka nchini.
Mabadiliko ya tabianchi yamekuwa tishio kubwa kwa wakulima wadogo katika maeneo ya mashariki mwa Gambia, ambapo ukame, dhoruba kali na mmomonyoko wa ardhi vimeathiri uzalishaji wa chakula na kipato cha jamii. Kupitia mradi unaoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEP) kwa usaidizi wa Green Climate Fund, wakulima wamepata mafunzo na msaada wa kitaalamu unaowezesha uzalishaji endelevu na kuongeza ustahimilivu dhidi ya athari za tabianchi. Hadithi hii inaangazia safari yao ya mabadiliko kutoka changamoto hadi mafanikio wakijenga mustakabali bora kupitia kilimo kinachohimili mabadiliko ya hali ya hewa.
Habari Nyinginezo
Afya
Kifua kikuu au TB bado ni moja ya magonjwa hatari zaidi ya kuambukiza duniani, kikiua zaidi ya watu milioni 1.2 na kuwaathiri takribani watu milioni 10.7 mwaka uliopita, kwa mujibu wa ripoti mpya ya kimataifa ya kifua kikuu 2025 iliotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO).
Tabianchi na mazingira
Wiki ya pili baada ya Kimbunga Melissa kupiga magharibi mwa Jamaica, mitaa ya Savanna-la-Mar na Watercress bado ipo kimya, kimya cha mji unaojaribu kujikwamua na Athari zilizoachwa na zahma hiyo. Nyumba zimebomoka, shule zimeharibiwa, maisha yamepinduliwa. Makadirio yanaonesha kuwa watu milioni 1.6 wameathirika, na sasa timu za misaada zinafanya kazi kwa haraka usiku na mchana kutoa msaada muhimu wa chakula, makazi, na usalama.