Vichwa vya Habari
Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Amani na Usalama
Kuanzishwa kwa ujumbe wa kitaifa wa msaada wa usalama nchini Haiti kutajadiliwa wiki hii na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wakati taifa hilo la Caribbea likiendelea kukabiliwa na mzozo wa ghasia na ukosesefu wa usalama unaosababishwa na magenge ya kiharifu ambayo yamekita mizizi katika nchi hiyo.
Habari kwa Picha
Umoja wa Mataifa: Kitovu cha diplomasia ya dunia
Viongozi kutoka kote ulimwenguni walirejea katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani katika mkutano wa kwanza kabisa wa ana kwa ana tangu janga la COVID-19 kuikumba duniani, na wameshiriki katika wiki ya kwanza ya mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa au UNGA78.
Habari Nyinginezo
Amani na Usalama
Watu wachache wanaokisiwa kuwa kati ya 50 hadi 100 kutoka jamii ya asili raia wa Armenia wameripotiwa kusalia katika eneo la Karabakh nchini Azerbaijan baada ya msafara wa siku za hivi karibuni kushuhudia zaidi ya watu 100,000 wakilikimbia eneo hilo, umeripoti leo ujumbe wa Umoja wa Mataifa ambao umefika eneo hilo kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 30.
Wahamiaji na Wakimbizi
“Safari ilikuwa ngumu sana, tulikuwa barabarani kwa saa kati ya 26 hadi 29.” Ni simulizi ya mmoja wa wakimbizi zaidi ya 100,000 wanaomiminika Armenia wakitokea eneo la Karabakh linalozozaniwa kati ya Armenia na Azerbaijan.