Vichwa vya Habari
Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Masuala ya UM
Je, itachukua nini kwa Palestina kuwa Nchi Mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa? Wakati Baraza la Usalama linashughulikia suala hilo wakati vita vya uharibifu huko Gaza vikiingia mwezi wake wa saba, tuliangalia hali ya sasa ya Palestina na kile kinachohitajika kuwa Nchi Mwanachama wa Umoja wa Mataifa.
Habari kwa Picha
Sudan: Hadithi za maumivu na mateso katika mwaka wa vita
Soha na Suhaila Ahmed, mwenye umri wa miaka 12, ni mapacha kutoka jiji la Nyala huko Darfur. Vita nchini Sudan viliwalazimu kutoroka pamoja na mama yao na mdogo wao hadi mji wa Port Sudan ulioko mashariki ya mbali ya Sudan, katika safari ngumu ya mabasi na malori ya mizigo, iliyochukua umbali wa kilomita 2,360. Wasichana hao wawili, mama yao mgonjwa, na mdogo wao wa kiume walipata makazi ya muda katika bweni la wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Port Sudan, wakisubiri kurejea Khartoum baada ya vita kuisha. Wasichana hao wawili wanangojea hatima isiyojulikana. Nilishangazwa na nguvu na uvumilivu wa wasichana hawa wawili na kwamba bado waliweza kutabasamu na kuwa na matumaini baada ya kupitia uzoefu huo mgumu.
Habari Nyinginezo
Haki za binadamu
Ripoti za kutisha zinaendelea kuibuka kuhusu makaburi ya halaiki huko Gaza ambako waathirika wa Kipalestina wameripotiwa kuvuliwa nguo wakiwa wamefungwa mikono, jambo ambalo limezusha wasiwasi juu ya uwezekano wa kuweko kwa vitendo vya uhalifu wa kivita huku kukiwa na mashambulizi ya anga ya Israel yakiendelea kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, OHCHR.
Haki za binadamu
Wataalamu wa Umoja wa Mataifa leo Aprili 22 wameelezea wasiwasi wao kuhusu jukumu la mashirika ya ndege na mamlaka ya usafiri wa anga katika kuwezesha kuondolewa kinyume cha sheria waomba hifadhi nchini Uingereza kuelekea nchini Rwanda kwa mujibu wa Mkataba kati ya serikali ya Uingereza na serikali ya Rwanda, na Muswada wa ‘Usalama wa Rwanda’.