Vichwa vya Habari
Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Masuala ya UM
Je, itachukua nini kwa Palestina kuwa Nchi Mwanachama kamili wa Umoja wa Mataifa? Wakati Baraza la Usalama linashughulikia suala hilo wakati vita vya uharibifu huko Gaza vikiingia mwezi wake wa saba, tuliangalia hali ya sasa ya Palestina na kile kinachohitajika kuwa Nchi Mwanachama wa Umoja wa Mataifa.
Habari kwa Picha
Sudan: Hadithi za maumivu na mateso katika mwaka wa vita
Soha na Suhaila Ahmed, mwenye umri wa miaka 12, ni mapacha kutoka jiji la Nyala huko Darfur. Vita nchini Sudan viliwalazimu kutoroka pamoja na mama yao na mdogo wao hadi mji wa Port Sudan ulioko mashariki ya mbali ya Sudan, katika safari ngumu ya mabasi na malori ya mizigo, iliyochukua umbali wa kilomita 2,360. Wasichana hao wawili, mama yao mgonjwa, na mdogo wao wa kiume walipata makazi ya muda katika bweni la wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Port Sudan, wakisubiri kurejea Khartoum baada ya vita kuisha. Wasichana hao wawili wanangojea hatima isiyojulikana. Nilishangazwa na nguvu na uvumilivu wa wasichana hawa wawili na kwamba bado waliweza kutabasamu na kuwa na matumaini baada ya kupitia uzoefu huo mgumu.
Habari Nyinginezo
Msaada wa Kibinadamu
Kufuatia tamko la serikali ya Sudan Kusini la kufuta uamuzi wake wa awali wa kutoza kodi malori yenye shehena za mafuta, Umoja wa Mataifa nchini humo umesihi kuachiliwa haraka kwa malori yake yaliyosheheni bidhaa hiyo pamoja na vifaa vingine muhimu.
Wahamiaji na Wakimbizi
Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu Volker Turk na Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Filippo Grandi hii leo wametoa wito kwa serikali ya Uingereza kufikiria upya mpango wake wa kuwahamishia nchini Rwanda wasaka hifadhi wanaofikia nchini humo.