Vichwa vya Habari
Chaguo la Mhariri
Makala Maalum
Afya
Aissata Touré, mwenye umri wa miaka 16, ndio kwanza amejifungua mtoto wake wa kwanza. Mama huyu ambaye naye ni mtoto, alikuwa na matumaini ya kjifungulia karibu na kijiji chao cha Ngouma nchini Mali, lakini mhudumu wa afya alimshauri aende hospitali kutokana na uwezekano wa kupata tatizo wakati wa kujifungua. Ilikuwa safari yenye changamoto na gharama kubwa.
Habari kwa Picha
Sudan: Hadithi za maumivu na mateso katika mwaka wa vita
Soha na Suhaila Ahmed, mwenye umri wa miaka 12, ni mapacha kutoka jiji la Nyala huko Darfur. Vita nchini Sudan viliwalazimu kutoroka pamoja na mama yao na mdogo wao hadi mji wa Port Sudan ulioko mashariki ya mbali ya Sudan, katika safari ngumu ya mabasi na malori ya mizigo, iliyochukua umbali wa kilomita 2,360. Wasichana hao wawili, mama yao mgonjwa, na mdogo wao wa kiume walipata makazi ya muda katika bweni la wanafunzi katika Chuo Kikuu cha Port Sudan, wakisubiri kurejea Khartoum baada ya vita kuisha. Wasichana hao wawili wanangojea hatima isiyojulikana. Nilishangazwa na nguvu na uvumilivu wa wasichana hawa wawili na kwamba bado waliweza kutabasamu na kuwa na matumaini baada ya kupitia uzoefu huo mgumu.
Habari Nyinginezo
Msaada wa Kibinadamu
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani WFP leo limetia saini mikataba miwili na Saudi Arabia yenye thamani ya dola milioni 1.4 ili kutibu na kuzuia utapiamlo nchini Sudan na Sudan Kusini.
Ukuaji wa Kiuchumi
Wiki ya uendelevu kwenye Umoja wa Mataifa imeingia siku ya pili hii leo ambapo mawaziri kutoka nchi mbali mbali wanachama wa Umoja wa Mataifa wamejinasibu ni kwa vipi sekta hiyo inaweza kuchochea mafanikio ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.